Friday, July 27, 2007

YANIPASA NIFANYE NINI NIPATE KUOKOKA?

Swahili

J.D. Phillips

1. MWAMINI Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako (Matendo 16:30,31). Lakini pasipo imani haiiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yoko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao (Waebrania 11:6). Aaminiye na kubatizwa ataokoka (Marko 16:16). Sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu (Yohana 8:24). Hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake. Yakobo 2:17).

2. TUBUNI mkabatizwe kila mmoja jina lake Yesu Kristu (Matendo 2:38). Lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo (Luka 13:3,5). Mungu ... sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu (Matendo 17:30). Mungu amewajalia hata mataifa nao toba liletalo uzima (Matendo 11:18).

3. Kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu (Warumi 10:10). Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu (Warumi 10:9). Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. (Mathayo 10:32). Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu akiye hai. (Mathayo 16:16). Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu (Matendo 8:37).

4. UBATIZO, unaowaokoa ninyi pia siku hizi (1 Petro 3:21). Aaminiye na kubatizwa ataokoka (Marko 16:16). Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu (Yohana 3:5). Kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu (Tito 3:5). Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu (Matendo 2:38). Simama, ubatizwe, ukaoshe dhambi zako (Matendo 22:16). Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo (Wagalatia 3:27). Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? (Warumi 6:3). Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya (2 Wakorintho 5:17).

5. TUPATE KUISHI KWA kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema. (Tito 2:12-14).

Nanyi mmeyashika yale mapokeo vile vile kama nilivyowatolea. (1 Wakorintho 11:2).

Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina. (Ufunuo 22:21).

Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. (Ufunuo 22:14).

Amina; na uje, BwanaYesu!

No comments: